MAN UNITED YAWACHAPA NOTTINGHAM FOREST 2-0


MABAO ya Antony dakika ya 32 na Diogo Dalot dakika ya 76 yameipa Manchester United ushindi wa 2-0 dhidi ya wenyeji, Nottingham Forest katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa The City Ground mjini Nottingham, Nottinghamshire.
Kwa ushindi huo, Manchester United imefikisha pointi 59 na kurejea nafasi ya tatu Newcastle United baada ya wote kucheza mechi 30, wakati  Nottingham Forest inabaki pointi zake 27 za mechi 31 nafasi ya 18.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post