KIKOSI cha Azam FC leo kimeanza mazoezi kujiandaa na mchezo wake ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Coastal Union Mei 24 Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
Huo ni mchezo mmoja kati ya miwili ya Azam iliyosalia, mwingine dhidi ya Polisi Tanzania Mei 28 Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam.
Mechi iliyopita Azam FC ilitandikwa mabao 2-1 na Namungo nyumbani Azam Complex.