NAIBU Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma ‘Mwana FA’ jana aliwafikisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa Yanga kuelekea mchezo wao wa marudiano Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika leo dhidi ya Marumo Gallants.
Yanga leo watakuwa wageni Marumo Gallants katika mchezo wa marudiano wa Nusu Fainali Kombe la Shirikisho Afrika Uwanja wa Royal Bafokeng mjini humo wakijitaji kuulinda ushindi wao wa nyumbani wa 2-0.