YANGA SC YAACHANA NA KIPA ERICK JOHOLA


KLABU ya Yanga imeachana na kipa wake nne, Erick Johola baada ya misimu miwili tangu awasili Jangwani akitokea Aigle Noir ya Burundi.
Erick Johola anakuwa mchezaji wa sita kuachwa Yanga baada ya beki, Abdallah Shaibu ‘Ninja’, kiungo Mzanzibari Feisal Salum aliyeuzwa Azam FC, mawinga Mghana, Bernard Morrison, Mkongo Tuisila Kisinda na mzawa, Dickson Ambundo.
Yanga pia imeachana na Kocha wake Mkuu, Mtunisia Nasredeen Nabi na Kocha wa makipa, Mbrazil Milton Nienov na kuajiri Kocha mpya, Muarngentina Miquel Angel Gamondi.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post