AZAM FC YAMTAMBULISHA MSHAMBULIAJI MPYA ALASSANE DIAO KUTOKA SENEGAL


KLABU ya Azam FC imemtambulisha mshambuliaji Alassane Diao kutoka US Goree ya kwao, Senegal. 
“Tunayo furaha kuwataarifu kuwa tumeingia mkataba wa miaka miwili na mshambuliaji hatari kutoka Senegal, Alassane Diao, akitokea US Goree,” imesema taarifa ya Azam FC.
Huyo anakuwa mchezaji mpya wa tatu tu Azam FC baada ya viungo mzawa, Feisal Salum Abdallah na Mgambia Djibril Silla.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post