ARSENAL YAICHAPA MANCHESTER CITY 1-0 EMIRATES


BAO pekee la Gabriel Martinelli dakika ya 86 jana liliipa Arsenal ushindi wa 1-0 dhidi ya mabingwa watetezi, Arsenal katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Emirates Jijini London.
Ushindi huo unaifanya Arsenal ifikishe pointi 20 katika nafasi ya pili, ikiizidi pointi mbili Manchester City huku ikizidiwa tu wastani wa mabao na vinara Tottenham Hotspur.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post