AZAM FC YATINGA NUSU FAINALI KOMBE LA KAGAME BAADA YA KUICHAPA LA MESSAGER NGOZI YA BURUNDI 1-0 CHAMAZI

 WENYEJI, Azam FC wamefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki ns Kati, maarufu kama CECAFA Kagame Cup baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Le Messager Ngonzi ya Burundi jioni ya leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Bao pekee la Azam FC leo limefungwa na winga wake, Iddi Kipagwile aliyerejea Chamazi baada ya msimu mmoja wa kucheza kwa mkopo Namungo FC ya Lindi dakika ya 22 akimalizia krosi ya chinichini ya Tepsi Evance.
Azam FC inafikisha pointi sita baada ya mechi mbili na inatangulia Nusu Fainali, wakati Messager inabaki na pointi yake moja kuelekea mechi za mwisho Jumamosi. GONGA HAPA KUTAZAMA VIDEO YA GOLU




Post a Comment (0)
Previous Post Next Post