SIMBA SC YATAMBULISHA MMALAWI MWINGINE, HUYU NI KIUNGO DUNCAN NYONI KUTOKA SILVER STRIKERS YA LILONGWE

MABINGWA wa Tanzania, Simba SC wamemtambulisha kiungo wa kimataifa wa Malawi, Duncan Nyoni kutoka klabu ya Silver Strikers ya kwao, Lilongwe kuwa mchezaji wao mpya wa tatu kuelekea msimu ujao.
Nyoni mwenye umri wa miaka 23 tu anakuwa Mmalawi wa pili kusajiliwa Simba SC dirisha hili baada ya winga Peter Banda kutoka Nyasa Big Bullet ya kwao pia, Blantyre.
Wamalawi hao wanafanya idadi ya wachezaji wapya waliotambulishwa Simba SC kufika watatu hadi sasa baada ya winga mzawa, Yussuf Mhilu kutoka Kagera Sugar ya Bukoba.

Bila shaka, Nyoni anakuja kuziba pengo la kiungo Mzambia, Clatous Chama anayehamia RSB Berkane ya Morocco kama ambavyo Banda amesajiliwa kwa sababu nyota wa Msumbiji, Luis Miquissone anahamia Al Ahly ya Misri.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post