TWAHA KIDUKU AMSHINDA TENA DULLAH MBABE KWA POINTI NA KUZAWADIWA GARI

 

BONDIA Twaha Kassim Rubaha ‘Twaha Kiduku’ ameendeleza ubabe kwa rafiki yake, Abdallah Shaaban Pazi ‘Dullah Mbabe' baada ya kumshinda kwa pointi usiku huu ukumbi wa Ubungo Plazza Jijini Dar es Salaam.
Kiduku alianza vibaya pambano hilo baada ya kuangushwa raundi ya kwanza tu, lakini akainuka na kumalizia raundi baada ya kuhesabiwa na refa.
Kutoka hapo Kiduku alitawala pambano kwa raundi zote tisa zilizofuatia na majaji wote wakampa ushindi wa pointi 98-91. wamepima uzito leo tayari kwa pambano lao kesho ukumbi wa Ubungo Plazza, Dar es Salaam.
Kwa ushindi huo, pamoja na malipo ya kawaida lakini Kiduku amekabidhiwa gari aina ya Toyota Crown Athlete. Hilo lilikuwa pambano la tatu baina yao kufuatia kutoka droo Oktoba 21, mwaka 2017 ukumbi wa Msasani Club kabla ya Kiduku kushinda kwa pointi Agosti 28, mwaka jana Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.




Post a Comment (0)
Previous Post Next Post