MAN UNITED YAAMBULIA SARE KWA SPURS 2-2 LONDON


TIMU ya Manchester United imetoa sare ya kufungana mabao 2-2 na Tottenham Hotspur katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa Alhamisi Uwanja wa Tottenham Hotspur Jijini London.
Man United ilitangulia kwa mabao ya Jadon Sancho dakika ya Marcus Rashford dakika ya 44, kabla ya Spurs kuzinduka kwa mabao ya Pedro Porro dakika ya 56 na  Son Heung-Min dakika ya 79.
Kwa matokeo hayo, Man United inafikisha pointi 60 katika mchezo wa 31, ingawa inabaki nafasi ya nne ikizidiwa pointi mbili na Newcastle United ambayo pia imecheza mechi moja zaidi, wakati Spurs yenye pointi 54 za mechi 33 sasa ni ya tano ikiizidi tu wastani wa mabao Aston Villa.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post