Mabao ya Arsenal yamefungwa na Martin Odegaard dakika ya 14 na Fabian Schar aliyejifunga dakika ya 71.
Kwa ushindi huo, Arsenal inafikisha pointi 81 katika mchezo wa 34 ingawa inabaki nafasi ya pili ikizidiwa pointi moja na mabingwa watetezi, Manchester City, ambao pia wana mechi moja mkononi.
Kwa upande wao, Newcastle United inabaki pointi zake 65 za mechi 34 nafasi ya tatu.