WACHEZAJI wawili wa Azam FC, Prince Dube Mpumelelo na Abdul Suleiman Sopu watachuana na wa Yanga, Bakari Mwamnyeto, Clement Mzize na Fiston Kalala Mayele kuwania Tuzo ya Mchezaji Bora wa Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC).