MTANZANIA KUWA KAMISHNA FAINALI LIGI YA MABINGWA AFRIKA


SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limemteua Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Mtanzania, Ahmed Mgoyi kuwa Kamishna wa mchezo wa Fainali ya Ligi ya kwanza ya Mabingwa Afrika baina ya wenyeji, Al Ahly dhidi ya Wydad AC Morocco Juni 4 Uwanja wa Cairo International Jijini Cairo nchini Misri.
Ahmed maarufu kama Msafiri Mgoyi ni Mjumbe wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na Mwenyekiti wa Chama cha Soka Kigoma (KRFA) na mmoja katí ya viongozi wasoefu wa Soka nchini.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post