NABI: MECHI YA KESHO INAHITAJI AKILI NYINGI NA TAHADHARI KUBWA

KOCHA Mtunisa wa Yanga, Nasredeen Nabi amesema kwamba mechi ya kesho dhidi ya Marumo Gallants ya Afrika Kusini inahitaji akili na tahadhari kubwa sana ili kupata matokeo mazuri.
Yanga SC watakuwa wenyeji wa Marumo Gallants ya Afrika Kusini kesho katika mchezo wa kwanza wa Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika kunzia Saa 1:00 Uwanja wa Benjamín Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Timu hizo zitarudiana Mei 17 Uwanja wa Venue Royal Bafokeng, Phokeng, NW na mshindi wa jumla atakutana na mshindi wa jumla kati ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast na USM Alger ya Algeria katika Fainali zitakazopigwa Mei 28 na Juni 3.




Post a Comment (0)
Previous Post Next Post