REAL MADRID YALAZIMISHWA SARE 1-1 NA MAN CITY BERNABEU


MABINGWA watetezi, Real Madrid wamelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Manchester City katika mchezo wa kwanza wa Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku huu Uwanja wa Santiago Bernabéu Jijini Madrid, Hispania.
Ni wenyeji, Real Madrid waliotangulia kwa bao la nyota wake Mbrazil, Vinícius Júnior dakika ya 36 akimalizia pasi ya Mfaransa mzaliwa wa Angola, Eduardo Camavinga, kabla ya Mbelgiji Kevin De Bruyne kuisawazishia Man City dakika ya 67 akimalizia pasi ya Mjerumani İlkay Gündoğan.
Timu hizo zitarudiana Mei 17 Uwanja wa Etihad Jijini Manchester, England na mshindi wa jumla atakutana na mshindi wa jumla katí ya AC Milan na Inter Milan za Italia.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post