AZAM FC YAAJIRI MFARANSA WA PILI KOCHA WA FIZIKI


KLABU ya Azam FC imeingia mkataba wa miaka mitatu na Mfaransa, Jean-Laurent Geronimi kuwa Kocha wake wa Fiziki kuanzia msimu ujao 2023/24. 
Geronimi anatambulishwa siku moja tu baada ya Azam kumtambulisha Mfaransa mwingine, Bruno Ferry kuwa Kocha wake Msaidizi kwa mkataa wa miaka mitatu pia.
Wawili hao anakwenda kuungana na Kocha Mkuu, Youssouph Dabo, Kocha wa Makipa Khalifa Ababakar Fall na Ibrahim Diop ambaye ni Mchambuzi wa mechi (Video Analyst) wote kutoka Senegal pia.



Post a Comment (0)
Previous Post Next Post