BENKI YA CRDB YASAINI KUWA MSHIRIKA MKUU WA WIKI YA MWANANCHI


BENKI ya CRDB imeingia makubaliano na klabu ya Yanga kuwa mshirika wake rasmi kwenye tamasha lake la Wiki ya Mwananchi ambalo kilele chake kitakuwa Julai 22 siku ambayo timu hiyo itamenyana na Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini katika mchezo wa kirafiki Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Wiki hiyo Mwananchi itazinduliwa rasmi Julai 15 Jijini Mwanza ikipambwa na matukio mbalimbali ikiwemo burudani na kuanzia leo benki ya CRDB itakuwa ikiandikisha wanachama wa klabu hiyo.




Post a Comment (0)
Previous Post Next Post