MABINGWA watetezi, Mlandege SC wamefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi baada ya ushindi wa penalti 3-2 kufuatia sare ya bila mabao na KVZ leo Uwanja wa New Amaan Complex, ZanzÃbar.
Sasa Mlandege watasubiri kukutana na mshindi wa Robo Fainali ya pili baina ya Mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga na mabingwa wa Rwanda, APR zinazomenyana leo usiku hapo hapo New Amaan Complex.