SIMBA SC YAMALIZA NA SARE KOMBE LA MAPINDUZI


TIMU ya Simba SC imekamilisha mechi zake za Kundi B Kombe la Mapinduzi kwa sare ya bila mabao na APR ya Rwanda usiku huu Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzíbar.
Simba SC inamaliza kileleni mwa Kundi B kwa pointi zake saba, ikifuatiwa na Singida Big Stars pointi sita, APR pointi nne na zote zinafuzu Robó Fainali, wakati JKU iliyomaliza bila pointi inaaga mashindano.
Sasa Robó Fainali Simba itamenyana na Jamhuri Jumatatu Saa 2:15 usiku, Singida Fountain Gate na Azam FC Saa 10:15 jioni na APR na Yanga Saa Jumapili Saa 2:15 usiku, wakati mabingwa watetezi, Mlandege SC watamenyana na KVZ Saa 10:15 jioni.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post