AZAM FC WAMZAWADIA JEZI MPYA BOSI KAMPUNI YA BAKHRESA


MENEJA Mauzo na Masoko wa Azam FC, Tunga Ally, leo amemtembelea Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bakhresa Food Products, Salim Aziz na kumkabidhi zawadi ya jezi za msimu mpya za klabu hiyo.
Baada ya kumpatia zawadi hiyo, Salim Aziz, alielezea furaha yake huku akifurahishwa zaidi kwa ubunifu na ubora wa jezi zetu.


Katika hatua nyingine Salim Aziz, alitumia nafasi hiyo kuitakia kila la kheri Azam FC ili ifanye vizuri kitaifa na kimataifa kwenye msimu mpya unaotarajiwa kuanza Novemba 29 mwaka huu.




Post a Comment (0)
Previous Post Next Post