BAYERN WAICHAPA DORTMUND 3-1 KUTWAA SUPER CUP UJERUMANI


TIMU ya Bayern Munich jana imefanikiwa kutwaa  Super Cup ya Ujerumani baada ya kuichapa Borussia Dortmund 3-1 Uwanja wa Signal-Iduna-Park, Dortmund.
Mpoland, Robert Lewandowski mwenye umri wa miaka 32 aliifungia Bayern Munich mabao mawili dakika ya 41 na 74, lingine likifungwa na Mjerumani, Thomas Muller dakika ya 49, wakati la Borussia Dortmund lilifungwa na Mjerumani mwingine, Marco Reus dakika ya 64.



Post a Comment (0)
Previous Post Next Post