SIFAN HASSAN ASHINDA MBIO ZA MITA 1,500 OLIMPIKI

BINGWA wa dunia, Sifan Hassan amefanya majaabu asubuhi ya leo baada ya kushinda mbio za mita 1,500 kwenye Michezo Olimpiki licha ya kuanguka, aliinuka na kuendelea hadi kuongoza.
Sifan ameshinda licha ya licha ya upinzani mkali alioupata kwa Mkenya, Edinah Jebitok mwanzoni – ametumia muda wa dakika 4 na sekunde 5.17 na kutinga Nusu Fainali.
Baadaye leo Mholanzi huyo, Sifan Hassan atakwenda kukimbia mbio za 5,000 ambako atapambana na Mkenya mwingine, bingwa wa dunia mara mbili, Hellen Obiri kuwania Medali ya Dhahabu.



Post a Comment (0)
Previous Post Next Post