YANGA SC YAANZA NA SARE YA 1-1 KOMBE LA KAGAME IKIWA PUNGUFU DHIDI YA BIG BULLET YA MALAWI


WENYEJI, Yanga SC wamelazimishwa sare ya 1-1 na Nyasa Big Bullet ya Malawi katika mchezo wa ufunguzi wa Kundi A Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Yanga ilitangulia kwa bao la mshambuliaji Waziri Junior dakika ya nane kwa kichwa akimalizia krosi ya mchezaji mpya, Dickson Ambundo kutoka Dodoma Jiji FC.
Na Nyasa Big Bullet wakasawazisha dakika ya 
30 kwa penalti ya Chiukepo Msowoya kufuatia beki Abdallah Shaibu 'Ninja' kumchezea vibaya Mnigeria, Babatunde Aderpoje.
Yanga SC ilimaliza pungufu baada ya kipa wake, Ramadhan Awam Kabwili kutolewa kwa kadi nyekundu kufuatia kumuangusha Hassan Kajoke kwenye boksi dakika ya 89.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post