SIMBA SC YATOA SARE YA 2-2 NA WENYEJI FAR RABAT KATIKA MCHEZO WA KIRAFIKI KWENYE KAMBI YAO YA MOROCCO LEO

 MABINGWA wa Tanzania, Simba SC leo wametoa sare ya 2-2 na wenyeji, FAR Rabat katika mchezo wa kirafiki leo Jijini Rabat nchini Morocco.
Mabao ya Simba yamefungwa na viungo Hassan Dilunga dakika ya 54 na Papa Msenegal Ousmane Sakho dakika ya 81 baada ya FAR Rabat kutangulia kwa mabao ya Chabani dakika ya 14 na Abba dakika ya 26.
Simba SC imeweka kambi Rabat kwa zaidi ya wiki sasa ikijiandaa na msimu mpya, lengo lao kuendeleza mafanikio yao yaliyodumu kwa misimu minne iliyopita.




Post a Comment (0)
Previous Post Next Post