SIMBA SC YAWAPIGA BONGE LA BAO WAPINZANI WAO, YANGA KWENYE USAJILI WA NYOTA MMALAWI, PETER BANDA


MABINGWA wa Tanzania, Simba SC wamemtambulisha winga Mmalawi, Peter Banda kuwa mchezaji wao mpya wa kwanza kuelekea msimu ujao.
Banda aliyekuwa anacheza kwa mkopo Sheriff Tiraspol ya Moldova kutoka Nyasa Big Bullets FC ya kwao, Malawi alikuwa pia anawindwa na wapinzani wakubwa wa Simba nchini, Yanga.
Na Simba imefanya jitihada za kumpata kwa gharama zozote winga huyo kwa sababu iko mbioni kumuuza kiungo wake wa kimataifa wa Msimbuji, Luis Jose Miquissone kwenda Al Ahly ya Misri kwa dola za Kimarekani 900,000. GONGA HAPA KUTAZAMA VIDEO


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post