REFA Ahmada Simba wa Kagera amefungiwa mechi tatu kwa kosa kukubali bao la kuotea la kiungo Mzambia, Clatous Chama katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Mbeya Kwanza, Simba SC ikiibuka na ushindi wa 1-0 Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam Februari 3, mwaka huu.