YANGA WAPO SAFARINI, WANAKWENDA NIGERIA KWA KAZI YA JUMAPILI


WACHEZAJI wa Yanga Stephane Aziz Ki (kushoto) na Mudathir Yahya wakiteremka kwenye ndege Jijini Addis Ababa, Ethiopia walipowasili asubuhi ya leo wakitokea Dar es Salaam, tayari kuunganisha ndege kwenda Nigeria kwa ajili ya mchezo na wenyeji, Rivers United Jumapili.
Yanga itamenyana na Rivers katika mchezo wa kwanza wa Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika Jumapili Uwanja wa Godswill Akpabio International mjini Uyo huko Akwa Ibom Kusini mwa Nigeria, kabla ya timu hizo kurudiana Aprili 30 Dar es Salaam.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post