SIMBA SC WAONDOKA KWENDA LINDI NA MTWARA KWA SHUGHULI MBILI


KIKOSI cha Simba SC kimeondoka leo Dar es Salaam kwenda Ruangwa mkoani Lindi kwa ajili ya mchezo wake wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya wenyeji, Namungo FC Jumatano Uwanja wa Majaliwa.
Simba itaunganisha safari baada ya hapo kwenda Mtwara kwa ajili ya mchezo wa Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) dhidi ya Azam FC Jumatano.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post