XHAKA APIGA MBILI ARSENAL YAICHAPA WOLVES 5-0


KOCHA Mikel Arteta amemalizia vizuri Ligi Kuu ya England baada ya ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya  Wolverhampton Wanderers leo Uwanja wa Emirates Jijini London.
Mabao ya Arsenal yamefungwa na Granit Xhaka mawili dakika ya 11 na 14, Bukayo Saka dakika ya 27, Gabriel Jesus dakika ya 58 na Jakub Kiwior dakika ya 78.
Kwa ushindi huo, Arsenal inamaliza Ligi na pointi 84, nyuma ya mabingwa Manchester City wenye pointi nne zaidi, wakati Wolves wanamaliza na pointi 41 nafasi ya 13.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post