MAYELE ATOKEA BENCHI KUIFUNGIA DRC UGENINI KUFUZU AFCON


MSHAMBULIAJI wa Yanga, Fiston Kalala Mayele usiku wa jana ameifungia bao la pili Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ikiibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya wenyeji, Gabón katika mchezo wa Kundi kufuzu Fainali za Kombe la Marita ya Afrika Uwanja wa Franceville nchini humo.
Mayele alifunga bao hilo dakika ya 83 baada ya kumtoka beki wa Gabón na kufumua shuti lililomshinda kipa Jean-Noël Amonome, huku bao la kwanza la DRC likifungwa na mshambuliaji wa AEL ya , Aaron Tshibola dakika ya Cyprus.
Fiston Kalala Mayele mfungaji Bora wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara na Kombe la Shirikisho Afrika, alifunga baada ya kutokea benchi dakika ya 74 kuchukua nafasi ya Yoane Wissa wa Brentford ya England.
Kwa ushindi huo DRC inafikisha pointi saba na kupanda kileleni mwa Kundi I ikiizidi tu wastani wa mabao Gabón, wakifuatiwa na Sudan pointi sita na Mauritania pointi tano baada ya wote kucheza mechi tano.
Mechi za mwisho Septemba 4, DRC watakuwa wenyeji wa Sudan na Gabon watakuwa wageni wa Mauritania.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post