Shujaa wa Yanga leo ni mshambuliaji wa Kimataifa wa Zambia, Kennedy Musonda aliyefunga bao hilo pekee dakika ya 14 akimalizia kazi nzuri ya beki Mkongo, Djuma Shabani.
Pamoja na ubingwa wa Ligi Kuu na ASFC, Yanga pia ni washindi wa Ngao ya Jamii na washindi wa pili wa Kombe la Shirikisho Afrika, wakihitimisha msimu mzuri kwao kihistoria chini ya kocha Mtunisia, Nasredeen Nabi.