MAN UNITED YAWAKANDA VIBONDE SHEFFIELD UNITED 2-1 BRAMALL


TIMU ya Manchester United imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Sheffield United katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Uwanja wa Bramall Lane, Sheffield.
Mabao ya Manchester United yamefungwa na Scott McTominay dakika ya 28 na Diogo Dalot dakika ya  77, wakati la Sheffield United limefungwa na Oliver Robert McBurnie kwa penalti dakika ya 34 kwa penalti.
Kwa ushindi huo, Manchester United inafikisha pointi 15 na kusogea nafasi ya nane, wakati  Sheffield United inabaki na pointi yake moja nafasi ya mwisho kwenye ligi ya timu 20 baada ya wote kucheza mechi tisa.
 


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post