TWIGA STARS WAKIJIFUA KUJIANDAA KUIKABILI BOTSWANA WIKI IJAYO


WACHEZAJI wa timu ya taifa ya wanawake, 'Twiga Starst’ wakiwa mazoezini Uwanja wa Kituo cha Ufundi cha TFF, Kigamboni, Dar es Salaam kujiandaa na mchezo wa kwanza wa Raundi ya Pili kufuzu Olimpiki ya mwakani Paris dhidi ya Botswana Oktoba 26 Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam.
Timu hizo zitarudiana Oktoba 31, Uwanja wa Taifa wa Gaborone na mshindi wa jumla atakutana na mshindi wa jumla kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Afrika Kusini katika Raundi ya Nne. Kuna raundi ya Tano pia nay a mwisho na baada ya timu mbil zitaiwakilisha Afrika huko Paris.



Post a Comment (0)
Previous Post Next Post