PAMBA FC YATOA SARE NA MBEYA KWANZA 1-1 MTWARA


WENYEJI, Mbeya Kwanza jana wamelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Pamba FC ya Mwanza katika mchezo wa Ligi ya NBC Championship Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.
Kwa matokeo hayo, Mbeya Kwanza inafikisha pointi 17 baad aya kucheza mechi nane na kuendelea kuongoza Ligi ya NBC Championship ikifuatiwa na Ken Gold ya Mbeya pia yenye pointi 16 za mechi saba na Pamba FC pointi 15 mechi nane pia.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post