MABINGWA MLANDEGE SARE TENA, 1-1 NA VITAL’O KOMBE LA MAPINDUZI


MABINGWA watetezi, Mlandege FC wamekamilisha mechi mbili za Kundi A bila ushindi baada ya kutoa sare ya kufungana bao 1-1 na Vital’O ya Burundi leo Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzíbar.
Mlandege walitangulia kwa bao la kiungo Optatus Yustin Lupekenya dakika ya 45 baada ya kazi nzuri ya Mcolombia, Diego Fernando, lakini mshambuliaji Kessy Jordan Nimbona akaisawazishia Vital’O dakika ya 64.
Timu zote sasa zina pointi mbili bada ya kutoa sare katika mechi zao za kwanza pia, Mlandege na Azam FC na Vital’O na Chipukizi United.
Mechi nyingine ya Kundi A itafuatia Saa 2:15 kati ya Azam FC na Chipukizi United hapo hapo New Amaan Complex.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post