CHELSEA YAICHAPA LUTON TOWN 3-2 PALE PALE KENILWORTH


TIMU ya Chelsea imeibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya wenyeji, Luton Town katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Kenilworth Road mjini Luton, Bedfordshire.
Chelsea iliuanza vizuri mchezo kwa mabao mfululizo yaliyofungwa na Cole Palmer mawili dakika ya 12 na 70 na Noni Madueke dakika ya 37, kabla ya Luton Town kupata mabao yake kupitia kwa Ross Barkley dakika ya 80 na Elijah Adebayo dakika ya 87.
Kwa ushindi huo, Chelsea inafikisha pointi 28 katika mchezo wa 20, ingawa inabaki nafasi ya 10, wakati Luton Town inabaki na pointi zake 15 za mechi 19 nafasi ya 18 kwenye ligi ya timu 20.


Post a Comment (0)
Previous Post Next Post