FISTON KALALA MAYELE NDIYE MCHEZAJI MPYA WA KWANZA YANGA SC DIRISHA HILI LA USAJILI KUELEKEA MSIMU UJAO, NI MSHAMBULIAJI MKONGO ANATOKA AS VITA YA KINSHASA


KLABU ya Yanga imemtambulisha mshambuliaji Mkongo, Fiston Kalala Mayele kuwa mchezaji wake mpya wa kwanza dirisha hili la usajili kuelekea msimu ujao.
Mchezaji huyo kutoka AS Vita ya kwao, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), amesaini mkataba wa miaka miwili kuungana na mabingwa hao wa kihistoria Tanzania.
Mayele anakutana tena na wachezaji wenzake wawili wa zamani wa AS Vita, kiungo Tonombe Mukoko na winga Tuisila Kisinda ambao pia ni Wakongo.



Post a Comment (0)
Previous Post Next Post